Find Us On Facebook
 
X

Monday 20 January 2014

STORI KAMILI ZA MSANII HUYU WA BONGO MOVIE "BASUPA" ALIYEVAMIWA KUPIGWA NA KUIBIWA NA VIBAKA...ANGALIA MAPICHA

Hii ni sehemu ya  taarifa zaidi kuhusu mwigizaji Basupa kuvamiwa usiku na watu wasiofahamika ambao walimpora.

Basupa ameanza kwa kusema>>’Dah mtu wangu yaani mi mwenyewe kwanza nilipagawa kwa sababu ilikua kama saa 6 usiku hivi,nimetoka homu kama kawaida nikasema ngoja nikatafute msosi,wakati natoa hela nilitoa 10,000 nikarudishiwa 5,000 kumbe wale jamaa walishatoka kupiga sehemu  nyingine washachukua simu wakawa wanakuja mitaa niliyokuwepo mimi’
‘Walipofika pale waliona kwenye mlango wa gari yangu nilipofungua waliona simu mbili,walichofanya wakati wanataka kuchukua simu ya pili wakafanikiwa kunipiga ngumi nikawa nimejing’ata sehemu ya mdomoni nikatoka pale mpaka kituo cha polisi wakanipa pf3 na Rb nikaenda Mwananyamala Hopital’
‘Niliporudi maskani tukachukua usafiri tukaanza kuwatafuta na tukafanikiwa kuwapata wawili tukawaleta hiki kituo cha Mwinjuma,wengine katika kuwahoji wakadai mpaka sa 10[Jan 19] mizigo yetu tutakua tumeipata kwa haraka haraka walikua kama 15.

‘Katika Group lao kuna watu kama 3 nikiwaona nawajua,hawakufanikiwa kuchukua chochote zaidi ya simu na pesa,kwenye gari tulikua watatu mimi na wasichana wawili,jamaa wanapatikana hapo mtaa wa Kichangachui ni hapa nyuma ya kituo cha Msaada Garage.


0 comments:

Post a Comment