Find Us On Facebook
 
X

Friday 7 February 2014

FAHAMU ALIPO MCAMEROON HUYU PEKEE ALIYEWAHI KUICHEZEA MAN UNITED



Eric-Djemba-Djemba
Huyu ndio mwafrika pekee kutoka katika nchi ya Afrika Magharibi – Cameroon ambaye amewahi kuvaa jezi ya klabu ya Manchester United.
Eric Djemba Djemba, kiungo mkabaji wa timu ya taifa ya Cameroon ‘The Indomitable Lions’, alipata bahati kubwa ya kuweza kusajiliwa na Manchester United mnamo mwaka 2003 akitokea klabu ya Nantes ya Ufaransa kwa ada ya uhamisho ya paundi million 3, alisajiliwa akitajwa kuja kuwa mrithi wa kiungo mahiri Roy Keane lakini baada ya muda mfupi tu alishindwa kufikia malengo kwa kuendekeza starehe na kushindwa kufanya kazi iliyompeleka Old Trafford.
article-2553508-1B3C46F100000578-504_634x435-1
Mwisho wa siku mcameroon huyo akauzwa kwenda Aston Villa ambapo napo alishindwa kung’ara na kuanza taratibu kupotea katika ulimwengu wa soka la kiwango cha juu.
Lakini baada ya kupotea kwa muda muda mrefu wiki hii kiungo huyo ambaye alifilisika amepata bahati ya kusajiliwa na timu St. Mirren inayoshiriki kwenye ligi kuu ya Scotland.
Djemba mabaye kwa sasa ana umri wa miaka 32, pia amewahi kuvichezea vilabu vya Odense na Burnley baada ya kutoka Aston Villa kabla ya kwenda Qatar na kisha Urusi.

0 comments:

Post a Comment