Find Us On Facebook
 
X

Tuesday 30 December 2014

Utafiti kuhusu athari za chumvi kwenye chakula .

Moja ya vitu ambavyo vimekuwa muhimu kwenye chakula cha mwanadamu ni chumvi ambayo hutumika kuongeza ladha ya chakula ambacho hutumika mezani . Umuhimu wa kiungo hiki umefikia hatua ya waswahili kuipbatiza chumvi jina la utani ambalo ni Mkuu Wa Jiko . Hata hivyo chumvi inaweza kuwa na madhara pale ambapo inatumika kuliko kawaida na madhara hayo ni kwa afya ya mtumiaji . Je chumvi ni mbaya kwa Afya yako? Mwili wa mwanadamu unahitaji chumvi kwa kiwango Fulani kwani inasaidia kuongeza mnadini ambayo mwili wako unayahitaji . Hatari ni pale unapokula chumvi nyingi kuliko kiwango ambacho mwili wako unahitaji . Imagundulika kuwa chumvi husababisha matatizo ya shinikioz la damu hali ambayo inaweza ikaongeza uwezekano wa mtu kupata matatizo ya shambulio la moyo pamoja na hatari nyingine za magonjwa ya moyo . Madaktari wanashauri utumiaji wa chumvi kwa kiwango cha chini ili kuepukana na matatizo haya . salt on food Je kiasi gani cha chumvi kinazidi kiwango cha kawaida . Kimsingi hupaswi kula zaidi ya gramu tano za chumvi kwa siku , hii ni sawa na kijiko kimoja cha chai ambacho kina ujazo wa milligram 5 . Kiwango hiki kinajumuisha chumvi ambayo unaongeza ukiwa unapika jikoni , chumvi unayoongeza mezani wakati wa kula na ile chumvi ambayo inapatikana kwneye chakula kiasili hii ni kwa sababu kuna vyakula ambavyo ndani yake kuna chumvi hata kama havina ladha ya chumvi . Mfano wa vyakula ambavyo tayari vina chumvi ndani yake ni Mikate , Sausage na nyama za kusaga , supu ya kutengenezwa kiwandani , vyakula vya nafaka ambavyo hutumika kwenye kifungua kinywa (breakfast) n ahata baadhi ya biskuti . Je tunatumia chumvi nyingi kuliko kawaida ? Waafrika wengi huwa na kasumba ya utumiaji wa chumvi kwa kiwango kikubwa kuliko kawaida na hii imezoeleka sana kuanzia majumbani mpaka mahotelini . Ni rahisi sana kutumia chumvi nyingi kuliko kawaida wakati wa milo ya kila siku . Nusu ya chumvi ambayo hutumiwa na watu ni chumvi inayopatikana kwenye vyakula hasa vile vya kutengenezwa viwandani ambayo huwekwa wakati wa utengenezaji wa vyakula hivi huko huko viwandani ili kuvifanya vikae kwa muda mrefu . Nusu nyingine ni ile ambayo ambayo huongezwa jikoni na ile ambayo watu huongeza mezani wakati wa kula ili kukoleza ladha ya chakula husika . Salt_Farmers_-_Pak_Thale-edit1 Nini kinatengeneza chumvi Chumvi inatengenezwa na vitu viwili ambavyo ni sodium na chloride , Sodium ni sehemu ya chumvi ambayo ambayo huongeza presha ya damu au kwa lugha inayoeleweka zaidi huongeza shinikizo au msukumo wa damu hasa pale unapotumia chumvi nyingi kuliko kiwango cha kawaida . Pamoja na ukweli kwamba tunatumia chumvi nyumbani , taarifa zinaoandikwa kwenye vihifadhi vya vyakula hasa vile ambavyo vinatengenezwa viwandani huonyesha kiwango cha madini ya sodium ambayo yametumika kwenye chumvi . Kijiko kimoja cha chai mara nyingi huwa kina miligramu 2000 za sodium . Ni jinsi gani tunaweza kutumia kiwango cha chini cha chumvi kwenye vyakula ? Haiwezekani kupunguza kiwango cha chumvi ndani ya siku moja au ghafla , mabadiliko yanapaswa kufanyika hatua moja baada ya nyingine . Muhimu ni kujizoesha hisia ya kudhani kuwa chakula kina ladha hata pale ambapo chumvi haijakolea Kama una kawaida ya kuongeza chumvi nyingi mezani hatua ya kwanza ni kuondoa kile kikopo kidogo cha chumvi mezani hasa wakati wa chakula , hii ni kwa sababu unapaswa kukumbuka kuwa kama ulishaongeza chumvi tangu jikoni hauna sababu ya kuongeza nyingine mezani . MSHARIQEN-7612-1 Jaribu pia kupunguza kiwango cha chumvi unachoongeza wakati wa mapishi yako , unapswa kuonja wakati ukiwa unapika ili kuepuka kuongeza kiwango cha chumvi ambcho kinaweza kuwa hatari kwa Afya yako . Kama chakula chako kina viungo ambavyo ndani yake kuna chumvi ya asili hupaswi kuongeza chumvi nyingine juu yake . Katika tafiti zilizofanyika hivi karibuni imefahamika kuwa kuna baadhi ya vitu vinavyoweza kutumika kama chuimvi ambavyo havna madhara sawa na ya chumvi kwenye mwili wa mwanadamu na mojawapo ni limao pamoja na ndimu . Kiungo kingine kinachoweza kuchukua nafasi ya chumvi kwenye chakula chako ni mdalasini . salt Vyakula visivyo na chumvi nyingi? Vyakula ambavyo havijatengenezwa kiwandani kwa maana ya vyakula halisi mara nyingi huwa havina chumvi nyingi na hii inamaanisha kuwa unapaswa kuchagua vyakula vya asili kuliko vile ambavyo vimetengenezwa viwandani . o-SALT-SHAKER-facebook

Monday 29 December 2014

Keith Millen meneja wa Crystal Palace?

Kocha wa muda wa timu Crystal Palace Keith Millen yuko tayari kuchukua jukumu la kuifundisha timu hiyo kama kocha wa kudumu. Millen anakaimu nafasi ya umeneja kwa muda baada ya kocha mkuu Neil Warnock kutimuliwa ,amekua na uzoefu wa kukiongoza kikosi hicho baada ya kufanya hivyo mara ya kwanza ni pale Tony Pulis alipoikacha timu hiyo mwanzoni mwa msimu. "Niko tayari kuwa kocha wa kudumu wachezaji wananiheshimu kwa ufahamu wangu, na kufanya kazi kwa bidii nimefanya hivi mara kadhaa pamoja nao". Pia kumekua na tetesi kocha Alan Pardew anaweza pewa nafasi ya kuwa kocha mpya katika klabu hiyo ya kusini mwa londoni.

Taarifa ya kinachoendelea hivi sasa kuhusu ndege iliyopotea jana Indonesia

majonziTaarifa zilizotoka muda mfupi uliopita kuhusiana na zoezi la utafutaji wa ndege iliyopotea ya AirAsia QZ 8501 zinasema kuwa vikosi vinavyohusika na utafutaji wa ndege hiyo vinasema kuna uwezekano mkubwa imezama kwenye kina kirefu cha bahari. Chanzo cha habari kutoka nchini humo kinasema uchunguzi kuhusu ndege hiyo bado unaendelea huku wakitumia ndege za kijeshi kutoka Indonesia na Singapore Kusini Magharibi mwa Pwani ya Borneo ambapo ilipoteza mawasiliano. kapt Rubani wa ndege hiyo Captain Iriyanto Bado jitihada za kuwatafuta abiria 162 waliokuwepo ndani ya ndege zinaendelea,na mpaka sasa hakuna mawasiliano yoyote,ilikua ikielekea Singapore. Shughuli ya kutafuta ndege ya AirAsia ambayo ilipotea jana Jumapili imeendelea leo tena baada ya kusitishwa kwa muda. Ndege hiyo ilikuwa safarini kwenda nchini Singapore ikitokea mji wa Surubaya nchini Indonesia na shughuli za kuitafua zinafanyika kwenye kisiwa cha Belitung. air

Hili ni dili analofungia mwaka 2014 msanii Davido

DavidO (1)Mwezi December ni mwezi ambao watu huwa wanafanya uchambuzi wa namna mwaka ulivyokwenda, kuangalia malengo ambayo umeyaweka yamepita au yamekwama na pia kuandaa mikakati mipya ya mwaka unaofuatia. Davido ni mmoja ya mastaa wanaomaliza vizuri 2014, amefanya vizuri kwenye muziki, siku ya December 27 alitoka na tuzo mbili kwenye AFRIMA Awards 2014, msanii Bora wa Mwaka na pia Hit Single yake ya ‘Aye’ kuwa wimbo bora wa mwaka. “JUST SIGNED A DEAL WITH CLOSE UP! GREAT WAY TO END THE YEAR!! NON STOP THANK YOU LORD!! #owonikoko”– @davidoofficial Hizo ni dalili njema kwa Davido 2015, tayari amesign dili ya kutangaza dawa ya mswaki ya Close Up, kasema ina mavuno ya Naira nyingi hivyo mbali na mauzo ya album aliyopanga kuitoa mwakani pamoja na deal nyingine ikiwemo ya shows, kupitia hii kajihakikishia mkwanja wa kutosha 2015.

Wakati wengine wakisherehekea kupata watoto…hali si shwari kwenye ndoa ya mchekeshaji maarufu Chris Rock

Wakati wengine wakisherehekea kupata watoto…hali si shwari kwenye ndoa ya mchekeshaji maarufu Chris Rock Posted by: Jesca TZA December 29, 2014 Ent. FILE: Comedian Chris Rock Has Filed For Divorce From Malaak Compton-RockMchekeshaji maarufu nchini Marekani Chris Rock ameamua kuachana na mpenzi wake wa siku nyingi Malaak Campton baada ya kudumu nae kwenye ndoa kwa miaka 19. Katika maelezo yaliyotolewa na mkewe Malaak alisema “baada ya mgongano mrefu na kudumu kwa miaka 19 katika ndoa yetu,Chris na mimi tumeamua kutengana na kila mmoja kufanya mambo yake”. rokMwanasheria wa mchekeshaji huyo Robert S.Cohen alithibitisha kupokea barua ya talaka toka kwa Kris kwenda kwa mkewe Malaak na kusema haya ni mambo binafsi na wahusika wameamua kuyafanya kwa usiri ili kulinda heshima ya watoto wao,”alisema Mwanasheria huyo katika moja ya jarida la nchini humo.

Tuesday 7 October 2014

KUHUSU OKWI KUPATA MAJERAHA

IMG_7819.JPG
Zikiwa zimebaki takribani mbili kabla ya mchezo wa watani wa jadi Simba na Yanga, daktari wa Simba SC, Yassin Gembe amesema kwamba mshambuliaji, Mganda Emmanuel Okwi aligongwa kwenye enka na goti katika mchezo dhidi ya Stand United, lakini yuko fiti kabisa kucheza Oktoba 18, dhidi ya Yanga SC.
Okwi alitolewa nje mara mbili kupatiwa huduma ya kwanza na Dk Gembe, lakini mara zote alirejea uwanjani kuendelea na mchezo.
Pigo la pili lilimfanya mchezaji huyo aendelee kucheza huku akichechemea, hali ambayo ilizua hofu labda amepata maumivu makubwa.
“Ni kweli Okwi aligongwa mara mbili,
mara moja kwenye enka na mara moja
kwenye goti. Lakini hayakuwa maumivu makubwa na ataendelea na mazoezi na wenzake” amesema Gembe
Aidha, Dk Gembe amesema kwamba
kipa Ivo Mapunda na beki Nassor
Masoud ‘Chollo’ wataanza mazoezi ya
kujiweka fiti wiki hii.
Ivo aliumia kidole na anatakiwa kuwa
nje kwa wiki nane, hivi sasa akiwa
yupo katika wiki ya tatu, wakati Chollo
aliyeumia mkono, anatakiwa kuwa nje
kwa wiki tatu, hivi sasa akiwa
anaingia katika wiki ya pili.
“Hawa wachezaji maumivu yao
hayawazuii kufanya mazoezi ya
kujiweka fiti, kwa hivyo niliwapa
mapumziko mafupi kabla ya kuanza
mazoezi ya kukimbia na gym. Ivo
nilimpa wiki mbili za kupumzika na
Chollo wiki moja, kwa hivyo wote wiki
hii wataanza mazoezi,” Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ na Haroun
Chanongo ambao wiki iliyopita
walifanya mazoezi mepesi, nao
wataanza mazoezi kikamilifu na
wenzao.
Majeruhi mwingine wa muda mrefu
Simba SC ni Mkenya, Paul Kiongera
ambaye anatakiwa kuwa nje kwa wiki
sita baada ya kuumia goti, hivi sasa
akiwa katika wiki ya nne- na Dk
Gembe amesema ‘fowadi’ huyo
anaendelea vizuri.

Monday 6 October 2014

MWANAFUNZI WA MIAKA 17 AMTUNDIKA MIMBA MWALIMU WAKE HUKO MKOANI RUKWA

WAKATI ikiwa imezoeleka kuwa baadhi ya walimu wa kiume huwarubuni wanafunzi wao wa kike na hata kuwaharibia kabisa ndoto zao za kielimu kutokana na kuwapa ujauzito, hali imekuwa tofauti mkoani Rukwa ambako mwanafunzi wa Kidato cha Pili anadaiwa kumzalisha mwalimu wake.
 
Mwanafunzi huyo aliyemzalisha mwalimu wake ana umri wa miaka 17, wakati mwalimu huyo anayefundisha katika Shule ya Sekondari ya Umma ya Nkasi, iliyopo mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Nkasi, Rukwa, ana umri wa miaka 25.
 
Tukio hilo linalotajwa kuwa la kwanza kutokea wilayani hapa, limekuwa gumzo kubwa kwa wakazi wa Nkasi na wilaya jirani.
 
Hata hivyo, kwa wanafunzi, wamekuwa wakimpongeza mwenzao kwa kujaliwa kupata mtoto katika umri wake huo mdogo, huku mzazi mwenzake akiwa na uhakika wa maisha kutokana na kuwa ni mtumishi serikalini.
 
Imeelezwa kuwa licha ya tukio hilo, mwalimu huyo aliyezaa na mwanafunzi wake bado anaendelea na masomo shuleni hapo, huku `mzazi’ huyo wa kiume akifundishwa na mzazi mwenzake.
 
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Namanyere hivi karibuni, Mkuu wa Shule ya Sekondari Nkasi mjini Namanyere ambayo ni ya mchanganyiko ya umma, Amiamie Nanga alisema mwalimu huyo alianza kazi shuleni hapo ikiwa ni mara yake ya kwanza kufundisha baada ya kuhitimu mafunzo ya ualimu chuoni.
 
“Yameshatokea, lakini haileti picha nzuri sana, lakini mimi nina uzoefu mkubwa na wakazi wa mwambao wa Ziwa Tanganyika, kwao si ajabu kuwa na uhusiano na watu waliowazidi umri, iwe kwa mtoto wa kike au wa kiume, wote ni sawa tu…
 
“Lakini katika kisa hiki, inaonesha walimu sasa wanapoteza haiba ya ualimu. Hii kazi ina miiko na maadili yake …kwa mwalimu huyu hii ni ajira yake ya kwanza, nikimaanisha ni kituo chake cha kwanza cha kazi tangu ahitimu masomo yake…” alisema.
  
 Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda alisema hakuna kosa kwa mwalimu huyo wa kike kwa kuwa tayari ni mtu mzima.
 
“Isitoshe katika kisa hiki ni nadra kumpata mlalamikaji … Mwalimu mwenyewe huyu wa kike hawezi kuwa tayari kujidhalilisha kuwa amebakwa, yalikuwa maamuzi yake.”
 
Aliongeza kuwa, kwa mwalimu huyo kupata ujauzito wa mwanafunzi wake hakuwezi kuathiri ajira yake, tofauti na mwalimu wa kiume akimpatia ujauzito mwanafunzi wake wa kike ambaye huathirika kwa kukatisha masomo.
 
Jitihada za kumpata mwalimu huyo wa kike na mwanafunzi huyo zimegonga mwamba baada ya watu wao wa karibu kumweleza  mwandishi  kuwa hawako tayari kuuzungumzia mkasa huo.
 
Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo waliohojiwa na mwandishi wa habari hizi kwa masharti ya kutoandikwa majina yao  kwa hofu ya kuchukuliwa hatua za kinidhamu shuleni hapo, pamoja na kukiri kutambua uhusiano baina ya mwanafunzi mwenzao na mwalimu wao, lakini walisema hivi sasa mwalimu huyo amesitisha uhusiano na mwenzao na kuanzisha uhusiano mpya na mwalimu mwenzao.
 
Walisema pamoja na mambo mengine ni kama mwanafunzi mwenzao ameathirika kisaikolojia baada ya ‘kupinduliwa’ na mwalimu wake wa kiume ambaye kwa sasa ndiye baba mlezi wa mtoto.
 
“Huyu mwalimu wa kike sisi sasa tunamwita shemeji yetu alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwenzetu… penzi lao lilikolea hadi sasa ameweza kumzalia mtoto huyo…, lakini kwa sasa inavyoelezwa ni kwamba penzi limehamia kwa mwalimu mwenzake,“ alisema mmoja wao.
 
Baadhi ya watu wa karibu na mwanafunzi huyo wanakiri kuwa mwanafunzi huyo hana uwezo wa kifedha kumudu kumpatia malezi stahiki mtoto wake huyo, hivyo hata mzazi mwenzake alipoanza uhusiano na mwalimu mwenzake hakuwa na jinsi, bali kukubaliana na matokeo.
 
“Usiniandike jina, sisi tunashauri mwalimu huyo wa kike na mpenzi wake huyo wa kiume ambaye ni mwalimu mwenzake wahamishiwe shule nyingine kwa sababu kama kioo katika jamii wameteleza kwa kiasi kikubwa na watashindwa kuwajenga na kuwalea wanafunzi wao kimaadili.
 
“Isitoshe tunajiuliza sheria hapa inasemaje maana kama angekuwa ni mwalimu wa kiume amempatia mwanafunzi wake wa kike ujauzito angeshitakiwa na kufikishwa mahakamani na pengine kuhukumiwa kifungo kisichopungua miaka 30 jela, sasa kwa hili sheria inasemaje?”Alihoji.
 
Baadhi ya wazazi mkoani hapa waliohojiwa na mwandishi kwa nyakati tofauti wameelezea kushangazwa na tukio hilo, na hasa kwa jinsi mwalimu alivyoshindwa kujizuia `kujiachia’ kimapenzi kwa mwanafunzi wake.

Credit: Habarileo

Rekodi 7 tofauti alizoweka Cristiano Ronaldo baada ya kufunga hat trick dhidi ya Bilbao

10649779_808787392518541_1971687263503280706_nMwanasoka bora wa dunia Cristiano Ronaldo jana usiku alifunga magoli matatu na kutimiza jumla ya magoli 17 katika michuano yote aliyoitumikia Real Madrid.
Magoli hayo yalimfanya Ronaldo aweke rekodi kadhaa kwenye historia ya soka na rekodi hizo zipo kama ifuatavyo:
*3 – Hii ni Hat trick ya 3 ya Ronaldo katika La Liga msimu huu na amefanikiwa kufunga hat tricks hizo katika kipindi cha siku 15 tu.
*111 – Mchezo wa jana usiku ulikuwa wa 111 kwa Ronaldo kuitumikia timu yake ya taifa au klabu na katika mechi hiz zote amefunga zaidi ya goli moja.
*Cristiano amekuwa mchezaji wa pili kufunga hat tricks 3 katika mechi 7 za raundi ya kwanza ya La Liga – baada ya Mariano Martin kufanya hivyo msimu wa 1943-44.
*Cristiano ndio mchezaji wa kwanza kufunga magoli 13 au zaidi katika mechi 7 za kwanza Liga – tangu alipofanya hivyo Echevaria katika msimu wa 1943. 
*50 – Cristiano Ronaldo mpaka sasa ameshatoa assists 50 kwa wachezaji wenzie wa Real Madrid.
*190 – Magoli matatu aliyofunga Cristiano Ronaldo jana dhidi ya Athletic Bilbao yalimfanya atimize jumla ya magoli 190 katika mechi 171 alizoichezea Real Madrid kwenye ligi.
*9 – Gareth Bale mpaka sasa amempa Cristiano Ronaldo assists nyingi kwenye La liga tangu mwanzo mwa msimu uliopita – amempata assists 9.

Abakwa akimtembeza Mbwa

Tuesday 8 July 2014

Kuhusu kuachiwa kwa filamu hii mpya kutoka nigeria

yello
Bodi ya filamu nchini Nigeria hatimaye imeidhinishwa kusambazwa kwa sehemu kubwa na kuonyeshwa kwa filamu hii kubwa barani Afrika Half of a Yellow Sun.
Awali Half of a Yellow Sun ilicheleweshwa na bodi hiyo na kufafanua sababu za kufanya hivyo kuwa ni kutokana na hali ya usalama inayoendelea katika nchi hiyo na kusema kuwa filamu hiyo inayoelezea vita vya wenyewe kwa wenyewe Nigeria ingeweza kusababisha machafuko.
yelo
Filamu hiyo kitabu chake kiliandikwa na mwandishi mahiri wa vitabu Chimamanda Adichie,
Hatua hiyo imekuja kipindi ambacho watengenezaji wa filamu hiyo ya Half Of A Yellow Sun tayari kuwa wameorodhesha kwa ajili ya kuonyeshwa nchini Marekani.

Kuhusu kipa Ochoa wa Mexico kuwa na vidole sita

BqWzg71CIAAhaGC
Katika michuano ya kombe la dunia kumeibuka wachezaji wengi ambao wameonyesha uwezo mkubwa kiasi cha kuteka hisia za watu wengi, mmoja wapo ni golikipa wa Mexico Guillermo Ochoa.
Golikipa huyu alionyesha uwezo mkubwa katika mechi alizoichezea Mexico kwenye michuano ya kombe la dunia inayoendelea nchini Brazil, kabla ya timu yake kutolewa na Uholanzi katika hatua 16 bora – lakini pamoja na kuondolewa kwa timu yake bado uwezo wake umeacha gumzo kubwa sana kwenye michuano hii.
Uwezo aliouonyesha Ochoa ulipelekea kuzuka kwa taarifa kwamba golikipa huyo wa Mexico aliumbwa akiwa na vidole sita vya mkononi. Zikatolewa mpaka picha kupitia vyombo vya habari mbalimbali ambavyo vilimuonyesha Ochoa akiwa na vidole sita.
06042250-f68e-11e3-b3a2-3503811abc43_AP962717263961
Lakini ukweli ni kwamba kipa huyo ambaye kwa sasa anawindwa na vilabu vingi hana vidole sita. Picha zilizoonyeshwa na kusambazwa kwenye vyombo vya habari ni za kutengeneza.

Thursday 1 May 2014

HABARI PICHAZ..MH. ZITTO ZUBERI KABWE AKILA NDIZI KUPINGA UBAGUZI WA RANGI...!



PICHAZ: YALIYOJILI MKUTANO WA UKAWA ZANZIBAR

 Umati wa Wazanzibar waliojitokeza katika mkutano wa Ukawa  Zanzibar.

Thursday 10 April 2014

WASHIRIKI WA REDS MISS UDOM 2014 WAPATA FURSA YA KUKUTANA NA BAADHI YA VIONGOZI WA NCHI DODOMA HOTEL


Reds Miss Udom walipata fursa ya kukutana na Naibu waziri wa Utamaduni na Michezo Juma Khamia Dodoma Hotel




Warembo wakiwa kwenye Pozi na Mh Juma Khamia na Baadhi ya waandaaji





baadhi ya waheshimiwa wakiongea na washiriki wa Reds Miss Udom

Sunday 2 March 2014

TAFADHALI PICHA ZINATISHA !! KUTANA NA WATU MASHUHURI WALIO MDHIHAKI MUNGU! NA MUNGU ALIVYOWAJIBU DHIHAKA ZAO!! BALAA!!



1. JOHN LENNON (MUIMBAJI)
Wakati alipokuwa akihojiwa na mwandishi wa habari wa gazeti la American alinukuliwa akisema hivi "Ukristo utakufa na kutoweka duniani, siwezi kuwa na wasiwasi na hilo kwa kuwa nina uhakika nalo. Mafundisho ya Yesu yalikuwa sahihi na wala sipingi hilo ila mafundisho yale yalikuwa mepesi sana ambayo mtu yeyote anaweza kuyafundisha. Hebu angalia leo, tumekuwa maarufu hata zaidi yake (Hapo alilitaja kundi lake la The Bettle).

Ilikuwa mwaka 1966.
Wiki moja baada ya kutamba kwamba yeye na kundi lake lilikuwa maarufu hata zaidi ya Yesu, akapigwa risasi sita na kufariki.

2. TANCREDO NEVES (RAIS WA BRAZIL)

Alisema kwamba endapo angepata kura laki tano kutoka katika uchaguzi mkuu wa Brazil na kuwa rais, hata MUNGU asingeweza kumtoa katika urais huo. Akafanikiwa, akapata kura zaidi ya hizo, akashinda uchaguzi, siku moja kabla ya kuapishwa, akafariki dunia.
 

3. CAZUZA (MWANAMUZIKI WA BRAZIL)
Alipokuwa katika shoo yake ndani ya jiji la Rio De Janeiro, alichukua sigara, akaanza kuivuta, akachukua nyingine na kisha kuirusha juu na kusema "Mungu, hiyo yako, chukua nawe uvute"

Alifariki akiwa na miaka 32 kwa ugonjwa wa kansa ya mapafu ambayo iliyaharibu sana mapafu yake kuliko mgonjwa yeyote yule. 
4. MTENGENEZAJI WA MELI YA TITANIC.
Baada ya kutengeneza meli ya Titanic, mwanahabari akamuuliza ni kwa kiasi gani ilikuwa salama nae akajibu "Ni salama sana, haiwezi kuzama na hata Mungu hawezi kuizamisha"
Nafikiri unajua kilichotokea kuhusu Titanic.
 

5. BON SCOTT (MUIMBAJI)
Mwimbaji huyu ambaye alitamba miaka ya 70 alitoa wimbo wake mmoja mwaka 1979 wenye maneno haya
"Don't stop me; I'm going down all the way, down the highway to hell'.

Tarehe 19 February mwaka 1980, alikutwa amekufa baada ya kupaliwa na matapishi yake.  
6. Mwanamke mmoja alikuwa akihofia sana kuhusu ulevi wa marafiki wa mtoto wake. Wakati wanataka kuondoka na gari, akamshika mtoto wake mkono garini na kumwambia "Binti yangu, Mungu awatangulie katika safari yenu" Yule binti akajibu "Gari imejaa mama, huyo Mungu labda akae kwenye boneti la gari".
Baada ya masafa fulani ya safari yao, gari lile lilipata ajali kiasi ambacho hata polisi hawakujua ni aina gani ya gari lilikuwa.
Lilikuwa limebondeka sana na watu wote walikutwa wamekufa. Kilichowashangaza polisi, trey la mayai wala halikuonekana kuguswa na hakuna hata yai moja lililokuwa limevunjika na wakati gari lilibondeka mpaka kutokutambulika.  
7. CHRISTINA HEWITT (MWANDISHI WA HABARI)
Huyu alikaririwa akisema hivi "Nimesoma vitabu vyote duniani, ila hakuna kitabu kibaya...kibaya na kibaya kama Biblia"
Siku chache baada ya kusema maneno hayo, mwili wake ulikutwa umeunguzwa na moto ambao haikujulikana mpaka leo ule moto ulisababishwa na nini.
 

8. MARILYN MONROE (MUIGIZAJI)
Huyu alifuatwa na Bill Graham na kumwambia kwamba alitumwa na Roho wa Mungu kwa ajili ya kumhubiria. Alimkaribisha ndani, akamsikiliza kwa makini, alipomaliza akasema "Simhitaji Yesu wako, unaweza kuondoka nae". Wiki moja baadae, alikutwa amekufa katika makazi yake. Polisi walijaribu kuchunguza kipi kilimuua, mpaka leo hawajapata jibu.  

Picha 7 kuhusu mauaji yaliyotokea kwenye kituo cha Treni China.

1T
aarifa iliyosambaa kwenye mitandao mbalimbali inasema kuwa kuna kundi la watu waliokuwa naPicha 7 visu limewashambulia na kuua watu 28 huku zaidi ya 100 wakijeruhiwa katika kituo cha treni kilichopo mjini Kunming nchini China.
6
Mashahidi wa tukio hilo wamesema kuwa washambuliaji hao walivalia nguo nyeusi na kuwavamia abiria waliokuwa wakingojea treni na kuwakatakata huku wengine wakiwadunga visu wale hasa walioshindwa kukimbia kwa kasi.
3
Polisi wamefanikiwa kuwauwa washambuliaji watano kati ya kumi waliofanya shambulio hilo,Shirika la habari la Xhinua limewalaumu watu wanaopigania kujitenga katika mkoa wa Shinjiang kwa tukio hilo,ulinzi bado umeimarishwa eneo la tukio.
2
4
5
7

Thursday 27 February 2014

The Game aweka wazi kuhusu uhusiano wake na Kim & Khloe Kardashian

gameKhloe Kardashian na The game walijiachia pamoja kwenye night club kiasi cha kuwapa watu mashaka kwamba  wawili hao wapo kwenye uhusiano wa kimapenzi hivi sasa.
Khloe alikuwa wa kwanza kukanusha uhusiano huo na kusema kwamba walikuwa wapo kwenye starehe kama marafiki.
Hivi karibuni The game amepata nafasi ya kuzungumzia kuhusu kile kilichotokea na ametoa exclusive mpya.
Akiwa kwenye radio ya BBC Radio1 Extra The game alisema asingeweza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Khloe kwasababu alikuwa na uhusiano na dada yake Kim kipindi kilichopita.
“Watu hawajui kuhusu mimi na Khloe kwamba tumejuana miaka 12 iliyopita. Nilikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Kim Kardashian kwa muda kidogo sana. Kanye West alikuwa bado mshkaji kipindi kile na hadi sasa bado ni mshkaji wangu na najua Kim anakaribia kuwa mke wake na tayari wanafamilia. Khloe pia ni mshkaji na tuko poa pamoja kwa hiyo hizo tetesi  kati yangu na Khloe hazina ukweli”
k

Maneno ya Diamond Platnumz kuhusu wasanii wanaomtengenezea ugomvi

Screen Shot 2014-02-27 at 9.37.36 AM

Staa huyu wa ‘Number 1 rmx’ ft Davido ameiandika hii na kuisambaza kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii ya Instagram na facebook.
Screen Shot 2014-02-27 at 9.36.11 AM

Ex-girlfriend wa Samuel Eto’o ashtua watu kuhusu umri wa mchezaji huyo.

hu
“Tatizo la Chelsea ni kukosa wafungaji, nina Eto’o ambaye ana miaka 32 au labda 35 nani anayejua?”.
Hiyo ilikua ni kauli ya kocha Jose Mourinho akimzungumzia Samuel Etoo na baadae mpenzi wa zamani wa Eto’o aliongea kuhusu umri wa mchezaji huyo kitu ambacho kimewashangaza watu wengi.
Anna Barranca alikuwa mpenzi wa zamani wa Eto’o na kupata mtoto mmoja wa kike ambaye hivi sasa ana miaka 11 amesema Eto’o ana miaka 39 kuelekea 40 na sio 35.
Mwanamke huyo amesema kwamba alijua kuhusu umri wa Eto’o wakati wapo Cameroon kutoka kwa mtu ambaye alikua pamoja na Etoo tangu utotoni.

P Square kuanzisha series yao mpya – The Alingo’s

2
Project hii imefanyiwa kazi kwa muda wa miaka 5 na mwaka huu ipo tayari kuanza kuonyeshwa, taarifa hii imetoka kwenye post ya Peter Okoye.
The Alingo’s ni TV series ya katuni ambayo stars wake ni Peter na Paul wakiwa kwenye muonekano wa katuni.
Project hiyo inasimamiwa na P Classic entertainment kampuni ambayo ipo chini ya P Square na kuongozwa na Peter Okoye.
Hii ni trailer ya series hiyo

Trailer....

Taarifa kuhusu kocha wa Taifa Stars kuachishwa kazi

Kim-PoulsenShirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen wamekubaliana kuvunja mkataba katika makubaliano ambayo ni siri kwa pande zote mbili.
Uamuzi huo umetangazwa leo (Februari 27 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kwa pamoja na Rais wa TFF, Jamal Malinzi na Kocha Poulsen mbele ya waandishi wa habari.
Rais Malinzi kwa niaba ya TFF ametoa shukrani za dhati kwa Kocha Poulsen kwa ushirikiano na mchango ambao ameutoa kwa Tanzania kuanzia kwenye mpira wa miguu wa vijana.
Naye Kim amewashukuru Watanzania kwa ushirikiano waliompatia kwa kipindi cha miaka mitatu alichokaa nchini kuanzia Mei 2011 alipoteuliwa kuwa kocha wa timu za Taifa za vijana, na baadaye Taifa Stars.
Akizungumzia benchi jipya la ufundi la Taifa Stars, Rais Malinzi amesema linatarajiwa kutangazwa hivi karibuni likiongozwa na kocha kutoka nje ya Tanzania.
Amesema kwa upande wa mechi dhidi ya Namibia itakayochezwa Machi 5 mwaka huu jijini Windhoek, Stars itaongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Ufundi, Salum Madadi akisaidiwa na kocha Hafidh Badru kutoka Zanzibar.
Katika hatua nyingine, Kocha Madadi amewaondoa wachezaji watano wa Yanga katika kikosi kilichotajwa awali ili wapate fursa ya kuitumikia timu yao kwenye mechi mbili za Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al-Ahly ya Misri.
Wachezaji hao ni Athuman Idd, David Luhende, Deogratius Munishi, Frank Domayo, Kelvin Yondani na Mrisho Ngasa. Pia kipa Ivo Mapunda ameondolewa katika kikosi hicho baada ya kupata msiba.
Nafasi zao zimezibwa na wachezaji Abdi Banda (Coastal Union), Himid Mao (Azam), Juma Luizio (Mtibwa Sugar), Said Moradi (Azam) na Shabani Kado (Coastal Union).
Taifa Stars itaingia kambini keshokutwa (Machi 1 mwaka huu) jioni kwenye hoteli ya Accomondia jijini Dar es Salaam, na itaondoka Machi 3 mwaka huu alfajiri kwa ndege ya South African Airways na kurejea nchini Machi 7 mwaka huu saa 8.15 mchana.

Wednesday 26 February 2014

Video inayosambaa ya Ostaz Juma akiombwa msamaha na Pnc.

21
Hii ni video ambayo imezunguka sana leo kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ambayo wadau wengi wa muziki wamedai ni kama kudharirishwa kwa wasanii wa Tanzania na kuonekana kama hawana msimamo na kazi yao waifanyayo.
31
Video hii inamunyesha memba wa zamani wa kundi hilo la Mtanashati Intertainment Pnc,akimuomba msamaha Big boss wa kundi hilo Ostaz Juma Namusoma.




Hii ndiyo status ya Kala Jeremiah iliyozua utata Facebook.

kalaa
Kwa kitu ambacho kinaonekana si cha kawaida kwa Kala Jeremiah kuandika status kali ikiwa kama inamchafua Diamond na kumsifia Ally Kiba kwa kile kilichosemekana kuwa Ally Kiba kakopa pesa ili kumalizia ujenzi wa nyumba aliyokuwa anajenga.
Screenshot_2014-02-26-13-09-30

Friday 14 February 2014

MAITI ZAKUTWA ZIMETELEKEZWA MUHUNGULA KAHAMA,TUNAOMBA RADHI KWA PICHA

Maiti zimekutwa zikiwa zimeteketea vibaya mjini kahama maeneo ya mhungula sababu ya maiti hizo bado ikiwa haijafahamika ni nini.



chanzo http://bundalawilliam.blogspot.com

MAGAZETI YA LEO VALENTINE DAY


.
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
mg16-w480-h580
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.